
Inasemekana kitu kinachoaminika kuwa
bomu la mkono kimetupwa kwenye Bar ya Arusha night park Mianzini wakati
watu wakitazama mpira.
Watu wa maeneo ya karibu kama Soweto walisikia mlio mkubwa
ulioambatana na taarifa ambazo bado hazijathibitishwa kwamba vimetokea
vifo na wengine wamejeruhiwa kwa kukatika mikono na miguu.
Usiku wa April 13 2014 kwenye baa iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini Arusha ambayo siku zote ni miongoni mwa sehemu zinazokua na mkusanyiko wa watu wengi kuanzia jioni, limerushwa bomu wakati watu mbalimbali wakitazama mpira.
Blog hii imepata nafasi ya kuongea na mkuu wa mkoa wa Arusha ambae ni kiongozi
wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ambae amethibitisha kwamba ni
watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Anasema
wote wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha bomu
hilo ni la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa hajajulikana
alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema hakuna aliepoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo uchunguzi wa awali umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa rasmi pale uchunguzi kamili utakapokamilika.
Usiku wa April 13 2014 kwenye baa iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini Arusha ambayo siku zote ni miongoni mwa sehemu zinazokua na mkusanyiko wa watu wengi kuanzia jioni, limerushwa bomu wakati watu mbalimbali wakitazama mpira.
Blog hii imepata nafasi ya kuongea na mkuu wa mkoa wa Arusha ambae ni kiongozi
wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ambae amethibitisha kwamba ni
watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Anasema
wote wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha bomu
hilo ni la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa hajajulikana
alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema hakuna aliepoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo uchunguzi wa awali umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa rasmi pale uchunguzi kamili utakapokamilika.








0 comments:
Post a Comment