Ads 468x60px

Sunday, April 13, 2014

DAKIKA 90 KATIKA VIWANJA VITATU ZIMEMALIZIKA, AZAM FC BINGWA, YANGA WA PILI, MBEYA CITY WA TATU

Dakika 90 za mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara katika viwanja vitatu tofauti zimemalizika huku Azam wakijihakikishia pointi tatu muhimu za kujitangazia ubingwa wa Ligi msimu huu wa 2014, kwa kuwabanjua Mbeya City mabao 2-1. na kufikisha jumla ya Pointi 59. Katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, Yanga wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Orjolo na kufikisha jumla ya Pointi, 55. na Mbeya City wanabaki katika nafasi ya tatu. Na katika Uwanja wa Taifa Ashant United wameifunga Simba bao 1-0.

*KUTOKA MBEYA AZAM 2-MBEYA CITY 1, YANGA WANAPATA MABAO 2 ORJOLO 1


Kutoka Mbeya, John Boko, anaipatia Azam bao la pili, na sasa Mbeya City 1 Azam 2. Kutoka Jijini Arusha Yanga 2 Orjolo 1, mabao ya Yanga yamefungwa na Zahri na Ngasa.
NA SUFIANI MAFOTO 

0 comments:

Post a Comment