
Mvua
zinazoendelea kunyesha mikoa tofauti Tanzania bado zimeendelea kuleta
madhara ambapo pamoja na taarifa ya Watanzania kadhaa kukosa makazi na
wengine kupoteza maisha bado barabara na madaraja vimezidi kubomoka.
Hizi picha ni za daraja la mto Mzinga ambalo ndilo linalounganisha
Dar na mikoa ya kusini limeanza kumeguka kufuatia mvua iliyonyesha na
inayoendelea kunyesha ambapo sasa Wasafiri wa kwenda Nachingwea, Masasi,
Tunduru, Mtwara, Lindi na maeneo jirani wamekwama.
Baadhi ya kampuni ambazo zinamiliki zaidi ya mabasi manne, zimekua
zikifaulisha wasafiri toka kwenye mabasi yaliyokwama upande wa Mtwara
kuingia kwenye basi lililo upande wa Dar na wa Dar kuingia basi la
Mtwara ili safari ziendelee.








0 comments:
Post a Comment