Ads 468x60px

Featured Posts Coolbthemes

Saturday, August 9, 2014

MAKAMU WA RAIS AIPA TUZO VETA KWA KUIBUKA WASHINDI WA KWANZA NANE NANE KITAIFA

 Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharibu Bilali akikabidhi tuzo ya Ushindi wa kwanza Kitaifa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kwa kuibuka washindi wa jumla katika Kundi la Taasisi za Utafiti na Mafunzo. Anaepokea ni Mkurugenzi Masoko, Mipango na Maendeleo,  wa VETA - Tanzania, Enock Kibendera

UNATAKA KUPUNGUA NA UMECHOSHWA NA UZITO/UNENE AMBAO KWAKO NI KERO!!

NIGHT OF HOPE 2014: BONGO FLEVA 1, BONGO MOVIES 0

Mchezaji wa Bongo Fleva, Ali Kiba akimtoka msanii wa Bongo Movies, Issa Mussa 'Cloud 112'.

WAZIRI WA UJENZI DK. MAGUFULI AIFAGILIA NSSF UJENZI WA DARAJA LA KIGAMBONI

WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, ameusifu Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kuhakikisha wanasimamia ujenzi wa daraja la Kigamboni.

Ujenzi wa daraja hilo umekamilika kwa asilimia 60 ambapo mpaka sasa NSSF imetoa sh. bilioni 117 kati ya Bilioni 214 zitakazokamilisha ujenzi wa daraja hilo.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam, alipotembelea daraja kuona namna ujenzi unavyoendelea, Dk. Magufuli alisema kuwa ujenzi wa daraja hilo umekutana na changamoto nyingi ikiwemo kina kilichokuwa katikati ya bahari kupoteza malighafi ya ujenzi ambapo wahandisi waliamu kufanya utafiti.

Alisema kuwa juhudi za NSSF  katika kufadhili mradi huo umewezesha changamoto zilizokuwa zikiukabili maradi huo kufanyiwa kazi.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa NSSF, Ludovick Mrosso, alisema kuwa mradi huo unatarajiwa kukamilika Julai, 2015 ambapo katika daraja zitakuwa barabara sita za magari, mbili za wapita kwa miguu.
Maradi huo unajengwa kwa kushirikisha Wizara ya Ujenzi, NSSF na Tanroads. 
Msafara wa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli ukiwa katika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Kigamboni linalojengwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa kushirikiana na Serikali.  

AJALI ENEO LA AFRIKANA, MBEZI BEACH MCHANA WA LEO

 Gari aina ya Nissan Hard Body yenye Namba za Usajili T 524 ALW likiwa limetupwa mtaroni na trela la lori (halipo pichani) ambalo lililigonga gari hilo na kutumbukia mtaroni eneo la Afrikana Mbezi Beach Mchana wa leo. Katika Ajali hiyo iliyohusisha Lori na gari aina ya Nissan Hard Body hakuna mtu yoyote aliyepoteza Maisha
 Wananchi wakisaidia Kulifunga minyororo gari aina ya Nissan Hard Body ambayo imetumbukia mtaroni mara baada ya Kugongwa na trela la lori (halipo pichani) mchana wa leo katika Eneo la Mbezi Afrikana
Wananchi wakisaidia kuligeuza gari ndogo aina ya Nissan Hard Body iliyotumbukia mtaroni eneo la Afrikana Mbezi Beach mara baada ya Kugongwa na trela la lori (halipo pichani) mchana wa leo, katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha. Picha zote na Josephat Lukaza Wa Lukaza Blog

ARGI + NA FAIDA ZAKE


MAONYESHO YA NANENANE NGONGO MKOANI LINDI

MCHUMI MKUU KUTOKA WIZARA YA FEDHA  ADAM  MSUMULE AKITOA MAELEZO KWA NAIBU KATIBU MKUU, WIZARA YA NISHATI NA MADINI,   INJINIA NGOSI MWIHAVA KATIKA VIWANJA VYA MAONYESHO YA NANENANE  NGONGO MKOANI LINDI.
WANANCHI WAKIMSIKILIZA KWA MAKINI JANET EZEKIEL, AFISA UHUSIANO WA PPF  KATIKA MAONYESHO YA KITAIFA YA NANENANE YANAYOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA NGONGO MKOANI LINDI.
AFISA MAWASILIANO NA  MASOKO RAHMA NGASSA  [KULIA] NA AFISA MFAWIDHI MKUU PSPF,  MTWARA OMARY KALILO [ KUSHOTO]  WAKISHUHUDIA MKUU WA WILAYA YA LINDI MJINI DKT. NASSORO ALI HAMIDI AKISAINI KITABU CHA WAGENI ALIPOTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA KATIKA VIWANJA VYA NANENANE NGONGO MJINI LINDI
ERICK MHOKOLE  MKUTUBI KUTOKA CHUO CHA MIPANGO DODOMA AKITOA UFAFANUZI KWA WANANCHI WALIOTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA MJINI LINDI KATIKA MAONYESHO YA NANENANE KITAIFA YANAYOENDELEA KATIKA VIWANJA VYA NGONGO.
NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA NISHATI NA MADINI  INJINIA NGOSI MWIHAVA AKISAINI KITABU CHA WAGENI KATIKA BANDA LA UTT ASSET MANAGEMENT , KULIA AFISA MASOKO NA UHUSIANO RAHIM MWANGA  AKITOA MAELEZO KWA WAGENI.
MENEJA  WA MKOA WA LINDI WA WAKALA WA HUDUMA YA UNUNUZI SERIKALINI [GPSA] , MWAKISELU MWAMBANGE AKITOA MAELEZO KWA MSHIRIKI ALIYETEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA KATIKA MAONYESHO YA KITAIFA YA  NANENANE  YANAYOFANYIKA NGONGO MKOANI LINDI.
MENEJA WA PPF KANDA YA KUSINI, ANTHONY NDADAVALA  AKITOA MAELEZO KWA WANACHAMA WA PPF WALIOTEMBELEA BANDA LA WIZARA YA FEDHA KATIKA MAONYESHO YA NANENANE YANAYOFANYIKA  NGONGO MKOANI LINDI.

Thursday, July 17, 2014

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2014 YATOKA

Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6 yaliyofanyika tarehe Mei 5 – 21, yametoka. Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa waliofanya mtihani kidato cha 6 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825.

Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420 sawa na asilimia 12.54
Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa na asilimia 1.74.

SHULE 10 ZILIZOONGOZA
1. Igowole
2. Feza Boys
3. Kisimiri
4. Iwawa
5. Kibaha
6. Marian Girls
7. Nangwa
8. Uwata
9. Kibondo
10. Kawawa

SHULE 10 ZA MWISHO
1. Ben Bella
2. Fidel Castro
3. Tambaza
4. MuhezaHigh School
5. Mazizini
6. Mtwara Technical
7. Iyunga technical
8. Al- falaah Muslim
9. Kaliua
10. Osward Mang'ombe
MATOKEO KIDATO CHA 6: 95.98% wafaulu kidato cha 6 kutoka 87.9% mwaka jana. Tambaza ndani ya shule 10 za mwisho, 
K/Katibu Mtendaji Necta 
C. Msonde 
 atangaza leo.

Feza Boys and Girls Secondary Schools emerge Top in Dar es salaam

The National Examination Council of Tanzania ( NECTA) has  released the Form Six National Examination results for 2014 indicating better performance over last year’s record.
The results from the examination sat on may this year showed  Feza Boys High school topping the lists of schools in terms of best performance in Daresalaam  and ranked 2nd nationalwise followed by the sister school Feza girls High school which became 2nd in Daresalaam and 12th nationalwise.
A  total of 60 candidates sat for the exam where 36 got division I, 18 students got division II and 6 students got division III which made the school 2nd nationalwise, and Feza girls had 41 candidates where 19 students got division I, 13 division II, and 9 division III’s .
The results further showed that Feza boys High school as the overall best school in science subjects as it topped chemistry, biology, history and Economics nationalwise.
The 2 students from Feza boys high school, Innocent Sabas Yusuf (3rd) and Ramadhan   Msangi(10th), managed to become among the top ten best students in Tanzania.

Since its commencement in the year 1998, Feza Schools have been pioneering provision of quality education to the Tanzanian Youth. From nursery, primary, secondary to high level education the school has established spacious compounds with home touch, teaching by Tanzanian curriculum for both boys and girls. 
Feza Schools have even recently opened an International school for both boys and girls, following the Cambridge Curriculum to suit more needs of the Tanzanians seeking for alternative education systems.

TAZAMA HAPA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2014

 

Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa waliofanya mtihani kidato cha 6 wamefaulu. 

Wasichana waliofaulu ni 12,080 na wavulana waliofaulu ni 26,825

Watahiniwa waliopata division IV ni 4,420 sawa na asilimia 12.54

Watahiniwa waliopata zero (0) ni 612 sawa na asilimia 1.74.

WAFUASI WA CCM,CHADEMA NUSURA WAZICHAPE KAVU KAVU MKUTANO WA NAIBU WAZIRI WA MAJI, AMOS MAKALLA

 Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan wa CCM (kulia), akiamulia ugomvi wa Diwani wa Kimara, Pascal Manota wa Chadema (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge waliotaka kuzichapa ulipotokea mzozo katika mkutano wa hadhara wa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla katika Uwanja wa Shule ya Mavurunza, Kata ya Salanga, Jimbo la Ubungo, Dar es Salaam jana.

TIMU YA AFRIKA YA KUSINI YAWASILI NCHINI KUIVAA SERENGETI BOYS JULAI 18

Kikosi cha Serengeti Boys.
Afrika Kusini (Amajimbos) imewasili nchini kuikabili Tanzania (Serengeti Boys) katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 itakayochezwa keshokutwa (Julai 18 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Timu hiyo yenye msafara wa watu 37 ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jana usiku (Julai 15 mwaka huu) na imefikia hoteli ya Sapphire. Amajimbos itafanya mazoezi leo saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Azam Complex.

Waamuzi watakaochezesha mechi hiyo kutoka Shelisheli wakiongozwa na Allister Barra tayari wamewasili nchini. Kamishna wa mechi hiyo ni Andriamiasasoa Doda Nirimboavonjy kutoka Madagascar.

Makocha wa timu za Seregenti Boys na Amajimbos pamoja na manahodha wao watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho (Julai 17 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).


Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000. Tiketi zitauzwa uwanjani katika magari maalumu siku ya mechi.

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA HABARI,VIJANA,NA MICHEZO AZINDUA RASMI KITABU CHA "HISTORIA YA KLABU YA SIMBA"KILICHOANDIKWA NA MWINA KADUGUDA

 Mwina Kaduguda Mtunzi wa kitabu cha "HISTORIA YA SIMBA" akielezea kwa kina Magumu gani amepitia wakati anaanza kuandaa kitabu hicho,Wa kwanza Kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mheshimiwa Juma Nkamia na Katikati ni Mkurugenzi wa Mkuki na Nyota Bwana Mkuki Bgoya ambao ndio wachapishaji wa kitabu hicho.Akielezea kwa ufupi Mwina Kaduguda amesema kwamba Dhumuni kubwa la Kutunga kitabu hicho ni kutaka kutunza historia ya soka ya Timu hiyo isipoteee ili iweze kusomwa kizazi na kizazi.

Msaada tutani: mtoto aibwa changanyikeni leo, ataemuona atoe taarifa polisi

MTOTO KAIBIWA CHANGANYIKENI LEO ANAITWA MARLYN.

ATAKAEMUONA NNAOMBA ATUSAIDIE KUTOA TAARIFA KITUO CHOCHOTE CHA POLICE. AMEIBIWA NA MKAKA KANYOA PANK. 

Please upatapo ujumbe huu mfowardie na mwenzako

KIPANYA LEO

Saturday, July 12, 2014

KONGAMANO LA NNE LA MAKATIBU MUHTASI TANZANIA (TAPSEA) LAFUNGULIWA LEO JIJINI MWANZA

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Mh. Dk. Mary Nagu akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la nne la Makatibu Muhtasi Tanzania,leo Julai 11,2013 jijini Mwanza.Mh. Nagu katika hotuba yake,amesema atawasimamia Makatibu hao na kuhakikisha wanaanzisha Benki yao ambayo itawawezesha kuweka abiba zao na kukopeshana pia.
 Mgeni Rasmi katika Kongamano la Makatibu Muhtasi Tanzania,Naibu Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Angela Kairuki akitoa hotuba yake katika ufunguzi wa Kongamano la nne la Makatibu Muhtasi Tanzania,leo Julai 11,2013 jijini Mwanza.Mh. Kairuki amewahimiza Makatibu Muhtasi hao kuhakikisha wanaudumisha na kuulinda umoja walionao,kwani umoja ndio msingi wa maendeo.
 Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania,Bi. Pilli Mpenda akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Mh. Dk. Mary Nagu pamoja na Mgeni Rasmi katika Kongamano la Makatibu Muhtasi Tanzania,Naibu Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Angela Kairuki wakati wa Kongamano la nne la Makatibu Muhtasi Tanzania,leo Julai 11,2013 jijini Mwanza.
Picha ya pamoja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA),Mh. Dk. Mary Nagu akifurahi jambo na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria,Mh. Angela Kairuki mara baada ya ufunguzi wa Kongamano la nne la Makatibu Muhtasi Tanzania,leo Julai 11,2013 jijini Mwanza.Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Muhtasi Tanzania,Bi. Pilli Mpenda. Picha na Othman Michuz

DAKTARI FEKI MWINGINE ADAKWA HOSPITALI YA RUFAA MOROGORO



Askari Polisi wakimtoa nje daktari feki, Karume Habibu (22) kutoka kwenye ofisi ya Mganga Mkuu wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ambako alihojiwa kabla ya kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi kwa mahojiano zaidi.

UNATAKA KUPUNGUA UZITO CLEAN 9 NDIO SULUHISHO LAKO!!


CLEAN 9 ni nini na ina nini??

Ina mchanganyiko wa bidhaa nne (Alovera Gel chupa 3, Ultra Lite, Bee pollen na Garcinia. Pia ina tape measure pamoja na chupa ya kupimia)

Ina kitabu cha muongozo wa jinsi ya kutumia.
CLEAN 9 ni muhimu katika kupunguza mwili kwasababu inafanya kazi ya kusaidia mfumo wako wa mmeng'enyo wa chakula,kuondoa sumu mwilini, kuondoa mafuta yaliyozidi mwilini na kukupa mfumo bora wa ulaji chakula.

Matumizi yake ni rahisi sana. Tumia bidhaa kwa usahihi kisha utahitaji kufanya mazoezi walau dakika 20 (kutembea,kuruka kamba,kukimbia au gym ukipenda), Kunywa maji ya kutosha angalau lita tatu kwa siku punguza au acha kabisa ulaji wa vyakula vyenye sukari,wanga na mafuta.

Unatumia kwa siku tisa na itakusaidia kupungua kilo 3 mpaka 8 na kupungua zaidi utatumia Nutri lean ambayo ina bidhaa za mwezi mzima na una uwezo wa kupungua kilo 10 mpaka 15...
Wasiliana nasi kwa mawasiliano hapo juu


NYUSI AJINADI KWA WANAMSUMBIJI WANAISHI ZANZIBAR

 Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akipokea zawadi kutoka kwa Jumuiya ya watu wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar.

Tuesday, June 24, 2014

CHEKI VIDEO YA NDOA YA LULU NA JOTI, KAA TAYARI COMMING SOON

RAIS KIKWETE KIKWETE AWAAPISHA BALOZI NA WAJUMBE WA TUME YA OPERESHENI TOKOMEZA IKULU DAR

Balozi Joseph Edward Sokoine akila kiapo,kupokea miongozo ya kazi na kupongezwa na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete leo amemwapisha balozi mmoja pamoja na wajumbe wanne wa Tume ya Operesheni Tokomeza katika hafla fupi iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam leo mchana.

Balozi aliyeapishwa ni Joseph Edward Sokoine ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.Wajumbe walioapishwa nia pamoja na Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Mstaafu Hamisi Amiri Msumi, Jaji Mstaafu Steven Ernest Ihema,Jaji Mstaafu Vincent Damian Lyimo pamoja na katibu wa tume hiyo Bwana Frederick Kapela.
 Wajumbe wa Tume ya operesheni Tokomeza wakiwakatika picha ya pamoja na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal (Wanne Kushoto) na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa pili kulia) wajumbe hao kutoka kushoto ni Katibu wa Tume hiyo Bwana Frederick Kapela Manyanda, Jaji Mstaafu Vincent Damian Lyimo(wapili kushoto), Jaji mstaafu Hamisi Amiri Msumi(Watatu kushoto), na Jaji Mstaafu Steven Ernest Ihema (kulia),Wasita kushoto ni  Balozi Joseph Edward Sokoine.
Picha ya pamoja na Balozi na Wajumbe wa Operesheni tokomeza. Picha na Freddy Maro

Friday, June 13, 2014

Magazeti Leo Ijumaa

1_c9cfc.jpg

KIPANYA LEO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDH MHESHIMIWA SAADA MKUYA SALUM (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2014/15

MHESHIMIWA SAADA MKUYA SALUM (MB), AKIWASILI BUNGENI MJINI DODOMA KUWASILISHA MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI  KWA MWAKA 2014/15 LEO. 

SOKO LA ILALA MCHIKICHINI JIJINI DAR LILIVYOTEKETEA KWA MOTO LEO

 Sehemu ya wafanyakazi wa Kikosi zimamoto wakiendelea na zoezi la kuzima moto ulioteketeza kabisa Soko la Ilala Mchikichini Jijini Dar es salaam leo.Moto huo ulianza majira ya saa sita usiku wa kuamkia leo na kuteketeza kila kilichokuwepo katika eneo la soko hilo. Chanzo cha kutokea kwa moto huo bado hakijajulikana mpaka sasa.Picha zote na Othman Michuzi.