Kikosi cha Serengeti Boys.
Afrika
Kusini (Amajimbos) imewasili nchini kuikabili Tanzania (Serengeti Boys)
katika mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa
vijana wenye umri chini ya miaka 17 itakayochezwa keshokutwa (Julai 18
mwaka huu) kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.
Timu
hiyo yenye msafara wa watu 37 ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere (JNIA) jana usiku (Julai 15 mwaka huu) na imefikia hoteli
ya Sapphire. Amajimbos itafanya mazoezi leo saa 10 jioni kwenye Uwanja
wa Azam Complex.
Waamuzi
watakaochezesha mechi hiyo kutoka Shelisheli wakiongozwa na Allister
Barra tayari wamewasili nchini. Kamishna wa mechi hiyo ni Andriamiasasoa
Doda Nirimboavonjy kutoka Madagascar.
Makocha
wa timu za Seregenti Boys na Amajimbos pamoja na manahodha wao watakuwa
na mkutano na waandishi wa habari kesho (Julai 17 mwaka huu) saa 5
asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000. Tiketi zitauzwa uwanjani katika magari maalumu siku ya mechi.









0 comments:
Post a Comment