Ads 468x60px

Sunday, April 13, 2014

Picha nyingine za Helikopta iliyoanguka na makamu wa Rais na kilichofanyika baada ya kuanguka tu.

Screen Shot 2014-04-13 at 1.55.22 PM 
Viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Gharib Bilal, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick na kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova walianguka na Helikopta hii asubuhi ya April 13 2014 kwenye uwanja wa ndege Dar.
Hitilafu ilisababisha helikopta kuanguka wakati ikipaa kuwapeleka kwenye maeneo mbalimbali yaliyoathirika na mvua zinazoendelea kunyesha ambapo hata hivyo walinusurika kifo isipokua majeraha madogomadogo tu.

Screen Shot 2014-04-13 at 1.55.45 PM
Screen Shot 2014-04-13 at 1.55.53 PM 
Kama unataka ripoti kama hizi zisikupite, jiunge na familia ya millardayo.com kupitia twitter instagram na facebook kwa jina hilohilo la MillardAyo ili niwe nakutumia kila ripoti inayonifikia.
Screen Shot 2014-04-13 at 1.55.08 PM
 Screen Shot 2014-04-13 at 4.37.13 PM
Taarifa iliyoifikia millardayo.com kutoka kwa mmoja wa Waliokuwemo kwenye Helikopta hii ya jeshi inasema wakati inapaa kwenye umbali wa kama futi tano hivi kutoka uwanja wa ndege Dar es salaam, ilizidiwa na upepo ulioirudisha nyuma na kuangukia paa kabla ya kutua chini.

Kilichofanyika ni watu waliokuwemo kutoka nje harakaharaka kisha aliekua akiiendesha kufungua tenki la mafuta na kumwaga mafuta yote alafu baada ya muda mfupi vikosi vya zimamoto vikaanza kuipiga maji helikopta hiyo ili kuepusha mlipuko.

Unaambiwa kama ingekua ni majira ya moto, helikopta hii ambayo ilikua inawapeleka kutazama maafuriko yaliyookana na mvua Dar es salaam ingeweza kuwa kwenye hatari zaidi ya kulipuka.

Screen Shot 2014-04-13 at 4.37.31 PM
Ndani ya Helikopta walikuwepo watu mbalimbali akiwemo Makamu wa rais Dr. Bilal, Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Mecky Sadick.

Kama unahitaji matukio kama haya yasikupite, jiunge na mimi kwenye twitter instagram na facebook kwa jina hilohilo la MillardAyo ili niwe nakutumia kila ripoti inayonifikia usiku au mchana.

Picha zote mbili kutoka http://nasmamafoto.blogspot.com/

0 comments:

Post a Comment